Spoken Word

Anaitwa Moi

 

NASKIA ANAITWA MOI

By Shesia the Poet

Haya Moi bila rungu hurumia walala hoi Maana wamechoka na wakiungana hutoboi Na hawatajali kama ni wa Bondo ama Sugoi Piga hatua za haraka wacha kuwa goigoi

Ni kubaya, sio mlima Kenya sio milimani Voi Sabina hajui acheke ama alie coz no more Joy Ju mali yake ilichomeka kwa lile soko la Toi Maskini anajaribu kujituma asife maskini

Na anapolalamika haskizwi kwa makini Wamekonda wengi they are getting more skinny Hivi mbona mnyonge hana haki!

Akiililia haki polisi wanamshika kwa hamaki!

Tena analimbikiziwa kesi za uongo baada ya kuwashtaki! Oyah skizeni kushikwa kiholela hatutaki!

Polisi tunawapenda ila vibaya mnatumiwa

Kuvuruga mikutano ndio mpate kusingizia watuhumiwa

D.O tumesubiri sana umalize mtu wa maziwa

Ama ilikuwa vice versa, kilio ni kwa watu wa miwa Tender ya kuimport sukari imepewa mheshmiwa Vijana wamerudi kukaa maskani

Ni wasomi ila wanatafuta kazi na hazionekani

Wenyu mumewapeleka wakasomee marekani

Idle youths mnawatumia kupora kwa maandamano ili mlaumu wapinzani

Azimio walisema inawezekana mkasema haiwezekani Eti hakuna mkate nusu mara pap mkawaita mezani Oh kidogo kidogo bipartisan ikawashinda mizani

Sahii wapo kimya ni kilio tu mashinaniTunaumia sisi kwa sisi wakutusemea nani

Bunge la mwananchi nalo lina vita vya fulani na fulani

Oyah wazalendo hizo mlianza ni gani

Mlijichimbia kaburi wenyewe haya fukieni mpande maua

Si mlisema my thief my choice” mbona mjute kuwachagua

Now hate yourself dont hate Ruto and gachagua

Tamu dole sambusa uamuzi wako usije kuua

Related posts
Spoken Word

BEAUTIFUL LIE

Spoken Word

PROMISES ZA HUSTLER

Spoken Word

Ni wewe naongelesha

Spoken Word

#RejectFinanceBill

Sign up for our Newsletter and
stay informed

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *