Spoken Word

THE ROTTEN SEED

Fumbo mfumbulie mjinga mwerevu alingamue

Ashakum si matusi so acha niwachanue,

Kuna wakulima wawili walikua na mbegu, dream zao zilikua ni wapate mazao sawa

Kampuni walikua nazo mbili na zote ziliahidi kuwapatia mbolea

Ili by the end of period X zile vitu walidream zingetimia

Mkulima akajiita mkutano, akapiga hesabu ni wapi angepanda mbegu

Na maybe angeongezea mbolea the seed ingenawiri na mazao angepata zaidi

Mashamba yakatayarishwa, mkulima akajituma, mbegu akaweka

Kampuni za mbolea zikajituma, maneno matamu pia wakatuma nayo watu waliotumwa kwa wakulima,

So mchanga ukachimbwa,mbegu ikatiwa kisha kufukiwa

Expectations zikiwa time ya kuvuna mkulima na familia ipate mazao ya kutosha leo kesho na hata milele. Na by the time wamwage mbolea, mbolea yenyewe ikue effective

Mvua ilipoanza kunyesha, ilikuja na fujo,

Kwanza kuosha mbolea

Pili kuchimbua mbegu, so ile ndoto ya kuchipuka na maybe mbegu kukua mti utakao faidi

Mkulima, watoto wa mkulima na watoto wa watoto wa mkulima iliishia

Time mvua ilinyesha.

Najua by 2027 tutakua na mashamba, lakini kurudia mbegu za 2022 itakua msiba wakujitakia

Nikweli tuliamini mbolea, but the truth is si mvua tu iliharibu mbegu but hadi mbolea ilichoma mbegu baada ya mvua kukatika,

Kampuni iliahidi chini ya siku kadhaa tungeona tofauti kwa mbegu zilizo wekwa mbolea

Miezi kadhaa imepita na hakuna dalili za mbegu kuchipuka

Ile mafuta ya sitini haijachipuka

Ilebima ya afya haija chipuka

Yule kijana kutoka slum atakaa kwa mlango juu ameshindwa na bei ya ufunguo wa maisha, education

Mwenye mbegu ni kila mkenya wa 18+, na mashamba ni zile sanduku hupangwa tukivote

Wenye mbolea forever itabaki kuwa chama na candidates wao

Its high time tukubali hakuna mtu atatulazimisha kupanda mbegu kwa shimo hatutaki

So in the meantime wacha tuzidi kuvuna mazao

Ule mti tulidhani ni mchenza, umegeuka kuwa m-ndimu

Related posts
Spoken Word

Nchi ya ahadi

Spoken Word

Swali

Spoken Word

THE MONSTER OF TODAY

Spoken Word

UNITE TO IGNITE

Sign up for our Newsletter and
stay informed

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *