Spoken Word

Mabeberu Weusi

By Shesia The Poet

Tunacelebrate mashujaa wa zamani , wenye walipigania uhuru na amani

But walituacha kwa hands za thieves dressed in suits  agenda yao ni

                         HI MONEY

Kuna brighter days kweli? Wacha tukeep Imani ,hakuna uhuru

So tunacelebrate our parents instead

The health workers wenye wamefight through thick and thin

Bila mshahara, wale wasanii wameshika upcoming artist mikono

Siasa place pia kwa kuonyesha youth kwa siasa your voice matters

Leo ndio tunacelebrate 60years of independence

But Kenyans hawachangamki, juu ya high pay tax

Wanaworry ni nini watakula adhuhuri

Waswahili husema not yet uhuru which is true

Kenyans wanalive in the past ,wanastruggle na neo-colonialism

NASKIA  SAUTI, NASKIA SAUTI

Naskia kilio cha mababu zetu walio pigania uhuru wa taifa hii

Kinaya ni kuwa uhuru tunaye licha ya sisi wananchi

Kukatwa ushuru wa hali ya juu

Wimbo wa mzungu aende ulaya mwafrica apate uhuru

(maumau) upo wapi kwa sasa

Viongozi waliutwa ulafi na kuwa mabeberu Weusi

Ni mara ngapi tumeskia mali ya umma imeibiwa

Msemo uliopo ni pesa kwa wazee  kazi kwa vijana

Miaka zaidi ya hamsini tangu nchi yetu kudaiwa k upata uhuru

Licha ya ufisadi kuwa hali ya juu

Ufisadi nchini imekua kama zao la fedha

Kila mwaka sisi husherekea siku kuu ya jamhuri na mashujaa

Ila ushawahi jiuliza pana shujaa yeyote katika enzi hii?

Wanasiasa ni wale wale ,miaka kumi uongozini

Hakuna maendeleo ,na ahadi waliyoahidi

Hakuna hata moja yaliyotimizwa na bado twasema tano tena

Ndugu zanguni wakenya ni lini tutakaa kufanywa vibonzo

Hebu tuamke na tukatae uongozi uliooza wakenya

Hebu tuamke na tukatae uongozi wa ukabila

Related posts
Spoken Word

Nchi ya ahadi

Spoken Word

Swali

Spoken Word

THE MONSTER OF TODAY

Spoken Word

UNITE TO IGNITE

Sign up for our Newsletter and
stay informed

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *