Spoken Word

JAMHOODIE

By A Zee Coptel

Nchi inahisi njaa na njeve,

Ipatie Jam-hoodie

Nchi imerudi kulewa ndio inaitwa Re-Pub-liq,

Jam alimarry Uri,ndio Jamhuri akazaliwa on 12th Dec 63,

Sahi ako 50+1 years na bado tuko minus,

Viongozi tumechagua I mean wenye Compyuta iliagua hawa mind about us,

Juliani ako njaa,

Na Walafi ndio wanatuongoza,

Bado tunakiss ass,

Mkololoni aliASSAsinate Kimathi ndio tunampea standing ovation,

Penye wakenya uenda vaccation free of charge miguu tupu,ye ni damu tupu iko kwa floor,amekanyanga red carpet kwa ocean!

Kama hio ndio ufalme basi wacha mbigu ibaki uko ujuu usishuke.

Tuko Huru?

Hatuko uhuru kenya,ata ukipewa Wing za Ereza Uwezi land in Berlin bila Visa!

Nchi yenye iko huru inapanga kuua Rais Mstaafu,

Inatoa kafara mbuzi, kondoo kuchoma mti kwa shamba alafu bado ugazzete holiday yakupanda miti😂

Unatupima sana.

Nchi haina uhuru ya chakula,

Nchi marks za mwanafunzi kcpe zinashindana bei ya unga si nchi yakujivunia,

Mahindi wanapanda,wanajivunia,wanauza nje ndio waimport tena

Alafu wanajivunia ati wanafanya maendeleo!

Nchi ukianza kumake pesa mingi kuliko rais,unaitwa statehouse unaekelewa mikono ka Butita na Njugush

Nchi unachagua Mbunge na hakusaidii

Zile vitu IEBC walituambia ndio zimetutoshanisha mbaya.

So nini yakujivunia na Pesa ya elino alimwaga kwa flood,kuna njeve wapee Jam-hoodie!

Related posts
Spoken Word

Nchi ya ahadi

Spoken Word

Swali

Spoken Word

THE MONSTER OF TODAY

Spoken Word

UNITE TO IGNITE

Sign up for our Newsletter and
stay informed

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *